Wednesday, January 17, 2018

JINSI UNASHIRIKI DHAMBI KUPITIA MIZIKI YA KIDUNIA.

Mwanamuziki mmoja aitwae Rihana, aliimba DIAMOND IN THE SKY! lakini cha kushangaza huwezi kukuta almasi(diamond) Angani.

Alikuwa anamaanisha nini sasa anaposema DIAMOND in the sky??

BIBLIA katika EZEKIEL 28:13, inasema, "Ulikuwa ndani ya adeni bustani ya Mungu,kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako,akiki,na yakuti manjano,na ALMASI,na zabarajadi,na shohamu, na yaspi,na Yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari."

KIINGEREZA inasema, "You were in Eden, the garden of God;
Every precious stone was your covering:
The sardius, topaz, and DIAMOND,
Beryl, onyx, and jasper,
Sapphire, turquoise, and emerald with gold.
The workmanship of your timbrels and pipes
Was prepared for you on the day you were created.

Shetani ndio kiumbe pekee anaetajwa kuumbwa kwa Almasi(DIAMOND).

Shetani ndio almasi anaekaa au ambae makazi yake yako mbingu ya pili.

Kila anaeimba na kuzishabikia nyimbo kama hizi,
Amini usiamini kwa kinywa chako unamkiri shetani na kujiungamanisha nae na kwa namna hiyo KUZIMU inakusubiri.

1 comment: