YEYOTE ULIEOKOKA ZINGATIA WEWE NI BARUA INAYOSOMWA NA WATU WOTE.
✔Kila mtu alieokoka Maandiko yanasema imempasa kuwa nuru kwa ulimwengu ili watu ambao hawajaokoka wakimwona wamtukuze Mungu lakini pia waokoke.
✴2wakorintho 3:2-3 "Ninyi ndinyi barua yetu,ilioandikwa mioyoni mwetu, inajulikana na kusomwa na watu wote......"
✔Lakini katika majira haya ya Laodikia kumekuwa na wimbi kubwa la wokovu vuguvugu kwa watu ambao wameokoka, wokovu umekuwa kitu cha kawaida kwao kiasi cha kushindwa kutofautisha waliookoka na wasiookoka.
✔Wokovu na viwango vya Mungu vya utakatifu havibadilishwi na mazingira yaliotuzunguka, kaka dada jihoji mwenyewe kama bado una wokovu uliupokea mwanzo au la!
✴Mpendwa katika jamii unayoishi unasomekaje? Watu wanauona wokovu ulionao au unalitukanisha jina Bwana!?
✴Binti ulieokoka mavazi unayovaa yanautangaza wokovu au unasomeka kama kahaba kwa mavazi yako yanayoacha sehemu zako kama matiti,mgongo,tumbo,mapaja wazi?
✴kijana unasomekaje unapokuwa chuoni au shuleni?
✴wazazi, mnasomekaje kwa watoto wenu?
✴waimbaji mnachokiimba mnakitenda? au mnaimba kwa desturi na mazoea tu?
✴wahubiri,wainjilisti,walimu,wachungaji tunasomekaje? Je,ni kweli Tunachokifundisha tunakiishi?
✔Kama mataifa watatusema watuseme kwa maisha Yetu kuwa na ushuhuda mzuri lakini ni fedheha mkristo ulieokoka mataifa wanakusema kwa⤵
🔹uzinzi na uasherati wako,
🔹umbea wako,
🔹uchonganishi wako n.k.
✔1PETRO 2:12 maandiko yanasema," Mwe na mwenendo mzuri kati ya mataifa,ili iwapo huwasingizia kuwa ni watenda mabaya,wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa".
✔Wewe ambae umeokoka lakini unadumu katika dhambi unamfanya Yesu aliekufa msalabani ni mpuuzi na watu wanautukana wokovu kwa sababu yako.
~Neno linasema katika 2TIMOTHEO 2:19," Lakini msingi wa Mungu uliobora umesimama,wenye muhuri hii,Bwana awajua walio wake.Na tena kila alitajae jina la Bwana na auache uovu."
✔Kama unajijua ni vuguvugu unachanganya masomo, duniani umo na kwa Mungu umo uwe na bidii UKATUBU kwa maana Vuguvugu wote watatapikwa watoke katika kinywa cha Bwana Yesu, NDIKO KUTAKUWAKO KILIO NA KUSAGA MENO!!
No comments:
Post a Comment