# HILI NI FUNDISHO_POTOFU.
Moja kati ya mafundisho potofu ni lile la kusema kuwa mtu AKISHAOKOKA, ameokoka moja kwa moja, Na mbinguni ataingia tu bila kujali atafanya dhambi tena.
Hili fundisho pia limezaa fundisho lingine la kusema wakati huu wa neema TUKO HURU ndani ya YESU ,tunaweza kufanya chochote MRADI tu tumeokoka.
Andiko moja wapo Wanalotumia ni YOHANA 10:28, "28 Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu."
Yohana 10 :28.
Yohana 10 :28.
Sasa, JE, NI KWELI MTU AKIOKOKA AMEOKOKA MOJA KWA MOJA BILA KUJALI ATAFANYA NINI?
JIBU NI HAPANA!!!
JIULIZE;
KWANINI YESU Alisema,WAITWAO ni wengi bali WATEULE ni wachache? { MATHAYO 22:14}.
KWANINI YESU alisema, Angalia Umekuwa mzima USITENDE DHAMBI TENA.{YOH 8:11}.
KWANINI YESU alisema, WAKWANZA watakuwa wa MWISHO? { MATHAYO 20:16}.
KWANINI BIBLIA Inasema , UTIMIZENI wokovu wenu kwa Kuogopa na kutetemeka.{WAFILIPI 2:12}.
KWANINI BIBLIA Inasema , mtu atakaeliharibu hekalu(mwili),Mungu atamuharibu mtu huyo {1WAKORINTHO 3:16}.
KWANINI YESU Alisema, HAKI yen isipozidi haki ya mafarisayo,HAMTAINGIA kamwe katika ufalme wa mbinguni.{ MATHAYO 5:20}.
KWANINI Maandiko yanasema kufanya dhambi baada ya kuokolewa ni kumsulubisha Mwana wa Adamu mara ya pili {EBRANIA 6:4-6}.
KWANINI biblia inasema tusafishe mwili roho na nafsi { 2Wakorintho 7:1}.
KWANINI YESU alisema, sio kila aniitae Bwana ataingia katika uzima {MAT 7:21-22}.
Kama Mchungaji wako,anakufundisha kuwa ukiokoka ndio basi umemaliza KILA kitu anakuandalia mazingira ya kukupeleka MOTONI, Maana yake atakuwa anakuhalalishia dhambi zote kwa kisingizio cha moyo Wako umebadilishwa basi mambo mengine hakuna shida.
Ni kweli YESU ameahidi uzima kwa wote waliookolewa, lakini lazima ufahamu HATA kama MUNGU ameahidi hivo,au Mungu akiweka Agano,Bado na wewe unasehemu ya kufanya ili kulikamilisha hilo Agano.
Waisrael katika safari yao ya kwenda kaanan, Lakini la kujiuliza ni kuwa je, Waisrael wote waliotoka MISRI walifika kaanani? Wote waliotamani mabaya na kwenda kinyume na maagizo ya Mungu waliangamizwa jangwani. Safari hii ni kielelezo cha safari Yetu ya Mbinguni.
YESU anasema Tuishi maisha matakatifu, tusiwasilikilize hao wanaotaka tusiishi maisha matakatifu katika mwili na roho.Yesu anasema wao wenyewe hawaingii hivo wasikuzuie na wewe usiingie.
1TIMOTHEO 4:1,
"1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;
1 Timotheo 4 :1.
1 Timotheo 4 :1.
Hakikisha unakuwa Mteule baada ya kuitwa, WATEULE ni wale tu ambao baada ya kuitwa ,wanaendelea kumtii Mungu na kumfata kwa kila NeNo.
KATIKA YOHANA 10:28, Yesu anasema, "
28 Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.
Yohana 10 :28.
28 Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.
Yohana 10 :28.
Hii Ni ahadi ya Yesu Lakini imeambatana na masharti, YOH 10:27. Ili usipotee na kupokonywa mikononi mwake ni LAZIMA KUIKIA SAUTI YAKE(NENO LAKE) NA LAZIMA KUMFUATA, vinginevyo lazima utapotea.
USIKUBALI KUDANGANYIKA.
Na, Isaiah Membe, mtumwa wa Kristo.
No comments:
Post a Comment