JEHANAM YA MOTO.
Walioko jehanamu wanajua tayari wameshapotea,wanajua hawana nafasi ya kuokoka kama ulionayo wewe,wanaelewa kabisa bila kumkubali yesu na kuokolewa na kuishi maisha matakatifu kwa watu walioduniani nao wataenda huko waliko.
Utampokea yesu lini ndugu yangu? Muda umeisha sasa wewe unaesoma ujumbe huu na bado hujaokoka kwa kumaanisha.
Ukifa dhambini hata kama unasali kanisa la kiroho utaishia motoni, kwanini usiokoke leo rafiki!? Walioko motoni wanakumbuka nafasi walizozichezea wakiwa duniani kama vile ambavyo umekuwa ukipuuza injili na maonyo unayokutana nayo.
Umekutana na neno mara ngapi linalokuonya juu ya dhambi, hata humu facebook ni post ngapi ambazo zimekuwa zinakuonya juu ya dhambi na kukutaka uokoke na kumwamini yesu lakini unaishia ku LIKE na ku COMMENT 'amen' kumbe ni mwathirika wa dhambi na huchukui hatua yeyote.
Rafiki yangu ninakupenda sitaki upotee milele ndio maana nakueleza haya ,sitaki uje ujute na kuzikumbuka post hizi ukiwa motoni ambapo majuto hayatakuwa na msaada tena kwako.
sasa kama utanipuuza nitakuwa nimefanya sehemu yangu nimemaliza na kumbuka wakati uliokubalika ndio sasa,siku ya wokovu ndiyo sasa 2WAKORINTHO 6:2. Mungu yuko tayari kukupokea kama utamgeukia leo.
Wakati tulionao ni wakati wa hatari siku tusioidhani Bwana wetu anarudi kuwachukua watakatifu. je,utakuwa miongoni mwao? Dhamiri yako inakushuhudia.
Kumbe si wakati wa kufanya mchezo na dhambi ni wakati wa kutubu na kurekebisha njia zetu na kuzidi kuomba neema ya kumaliza safari kwa ushindi.
Neema ya kristo iwe nanyi nyote.
No comments:
Post a Comment