Tuesday, January 16, 2018

WOKOVU NI BADILIKO LA WAZI

MTU AKIWA NDANI YA KRISTO AMEKUWA KIUMBE KIPYA, YA KALE YOTE YAMEPITA.

"Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya” (2Wakorintho 5:17)

“Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye KATIKA YEYE TUNA UKOMBOZI YAANI, MSAMAHA WA DHAMBI”.(Wakolosai 1:13,14).

Kumbuka;

(Warumi 8:1-2 )
"Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. 2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti."

Yohana 3:18
"Amwaminiye yeye (YESU KRISTO) hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu."

"Amwaminiye Mwana (YESU KRISTO ) yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia." (Yohana 3:36)

Unaweza kusema me tayari nimeshaokoka lakini kumbuka na kuzingatia hili, utakatifu/ukamilifu ni mwili na roho. (2wakorintho 7:1, 1wathesalonike 5:23, 1petro 1:15, Mathayo 5:48, Waebrania 12:14). Utakatifu ni pamoja na tabia zetu za nje, yaani miili yetu katika mavazi, mienendo,Maneno na usemi wetu n.k, Lazima tukae kwa haki bila lawama wala kulaumiwa katika roho na mwili..

Jihoji mwenyewe, je wewe ni mtakatifu wa mwili na roho??Majibu  dhamiri yako inasema wazi, kwa sababu maisha yako unayajua jinsi ambavyo hayana ushuhuda kwa waliokuzunguka kutokana na unavovaa, unavoongea, unavyoishi na watu, pamoja na kusema umeokoka.

Ni uamuzi wako!

Maandiko yanasema kuwa;

"Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako" (Matendo 16:31)

Yesu anabadilisha kabisa maisha ya mtu, inabaki historia na ushuhuda wa wazi kabisa unaonekana kwa wale wanaokufahamu. Kubali Yesu akubadilishe leo.

"Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka" (Warumi 10:9)

Ikiwa unasikia sauti ya MUNGU ndani ya moyo wako ikikuambia unahitaji kubadilika na kumpokeaYESU KRISTO basi kwa kinywa chako na kwa imani fuatusha maneno  haya;

"BWANA YESU,HAKIKA MIMI NI MWENYE DHAMBI, SIJAWA MTAKATIFU WA MWILI NA ROHO.
BWANA YESU NISAFISHE MOYO WANGU KWA DAMU YAKO, NIPE UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI ZOTE NA KUNIWEZESHA KUISHI MAISHA YANAYOKUPENDEZA WEWE. JINA LANGU LIFUTE KWENYE VITABU VYA HUKUMU NA ULIANDIKE UPYA KATIKA KITABU CHA UZIMA WA MILELE. NAJITOA KWAKO KUANZIA LEO UWE BWANA NA MWOKOZI WANGU, NIFANYE KUWA KIUMBE KIPYA SASA.AMEN."

Kama umetamka kwa imanina kudhamiria ndani yako, hakika Bwana amekusamehe. Lakini utahitaji msaada zaidi ili uendelee kudumu katika mafundisho ya usafi na utakatifu.

Kwa msaada zaidi wewe ambae unadhamiria kweli kuwa mtakatifu na kumuona Mungu, tafuta kanisa linalohubiri na kuzingatia utakatifu wa mwili na roho au waweza kunitafuta ili tuendelee kujifunza na kupata maelekezo mengine zaidi..

namba: 0764569023.

Isaya Membe, ndugu yako katika Kristo.

No comments:

Post a Comment