Wednesday, January 17, 2018

LENGO LAKO NI NINI?

LENGO LAKO NI NINI?

✔Ni kweli kabisa wanadamu tunawaza na tunamalengo mengi ambayo yanatofautiana kati ya mtu na mtu mfano Katika LUKA 12:16-21, tunaona mtu mmoja aliekuwa na lengo la kujiwekea akiba mavuno yake katika ghala kubwa asijue muda wake wa kuishi duniani umekwishaa.

✔pamoja na malengo yote tulionayo, ila lengo kuu ni kuupata uzima wa milele,hili ndio liwe la kwanza katika maisha yetu na hayo malengo mengine tutazidishiwa tu. MATHAYO 6:33.
✴Ukikosa uzima wa milele utakuwa umepata hasara ya milele.

✔Hakikisha jina lako limeandikwa kwenye kitabu cha uzima, hutaweza kuandikwa huko kama lengo lako kuu ni kuyapata yaliochini tu, wakati yote unayafikiri yaliochini (duniani).

✔Mtu mwenye lengo kuu la kuupata uzima wa milele anaweza kustahimili majaribu na mikikimikiki ya adui na hawezi kurudi nyuma hata akiyakosa haya madogomadogo.

✔Yesu Akasema itakufaidia nini ukiupata ulimwengu huu wote na ukapata hasara ya nafsi yako? Hakuna faida zaidi ya kuishia jehanam ya moto.

✔Kaka zangu,dada zangu bado kitambo kidogo tu YESU atakuja,wala hawatakawia LAKINI wanaositasita MUNGU hapendezwi nao
🔹wengine wanawaza ngoja niache wokovu kwa muda nitaokoka tena baadae.
✴rafiki Yesu akasema hatujui ni siku ipi wala saa ipi atakayokuja mwana wa adamu
🔹 Ni Muda mfupi sana umesalia, Yesu atakuja kulichukua kanisa,ni wale tu waliojiweka tayari kumsubiri Bwana wao.

✔watakatifu waliotutangulia waliutazamia mji ule wa mbinguni kwa imani, hata walipopita katika magumu hawakutetereka wala kubabaika, WAEBRANIA 11:8-10..

✔Hukumu haina huruma kwake Yeye asie na huruma, Yesu ametuokoa kwa upendo wake kwetu ili tusiangamie na anatutaka na sisi tuwahurumia wengine na kuwaleta kwake.
🔹kama hatushuhudii wengine habari njema,hatuwahubiri wengine waokoke, hatuwaaliki walisikie neno la Kristo,watuwaombei wengine,watuwafundishi wengine kama hivi mitandaoni nasi pia mbinguni hatutaingia.
✴BWANA AMPE NEEMA KILA MMOJA KUUKOMBOA WAKATI✴

No comments:

Post a Comment