Tuesday, January 16, 2018

TOBA NI KUMAANISHA KUACHA.

AFICHAE DHAMBI ZAKE HAWEZI KUPATA REHEMA KWA MUNGU.:

MITHALI 28:13

Watu wengi sana katika taratibu za madhehebu yao wanaungama kila  jumapili katika sala ya maungamo lakini ni kwa desturi na mazoea tu, Wala ndani yao hadhamirii kuacha dhambi. Watu wa jinsi hii hawawezi kupata rehema kwa Mungu wala maisha yao hayawezi kubadilika.

Wengine Watakuwa wanaenda wa kwa viongozi wa dini zao kuungama dhambi zao,Lakini watu hawa ni wanafiki kwa sababu utakuta wanaungama dhambi mbili tatu tu tena kwa desturi na mazoea tu.

MARCO 7:6-9.
"6 Akawaambia, Isaya alitabiri vema juu yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, Watu hawa huniheshimu kwa midomo Ila mioyo yao iko mbali nami;

7 Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu,

8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.

9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.

Ndio maana hakuna badiliko lolote lile la maisha yao baada ya hapo, kwa sababu hawana hata huo mpango wa kuacha dhambi. Anaungama ulevi ndani yake wala hana mpango wa kuacha ulevi n.K,  Huwezi kupata wokovu kwa staili hio hata kidogo.MITHALI 28:13.

Mungu  anasema, anaeungama dhambi na kuziacha huyo ndie atakaepata rehema tena tunatubu kwa Mungu moja kwa moja. WARUMI 10:9-10.

Tubu kwa kumaanisha kuacha, utapata rehema kwa Mungu itakayoambatana na uwezo wa kushinda dhambi zote. YOH 1:12.

Mwl. Isaiah Membe, mtumwa wa Kristo.

No comments:

Post a Comment