WOKOVU WA KUIGIZA.
✔kwa wale wote ambao wokovu wao ni wa jumapili tu, ikifika siku ya ibada unajifanya ni mtakatifu, unajifanya kuvaa mavazi yenye heshima ila ukitoka tu tayari unakuwa mbwa mwitu!!
Hayo yote unayofanya ndio, unaweza kumdanganya mchungaji wako, unaweza kuwadanganya washirika LAKINI YUKO MUNGU AMBAE NI MWISHO WA YOTE, HUWEZI KUMFICHA WALA KUMDANGANYA. Mungu kwake giza na nuru ni sawasawa.Hata ungejificha wapi macho ya Mungu kama mwale wa moto bado yatakuona tu!
✔Matendo yako yote record zake ziko mbinguni na siku inakuja Mungu atakapozifuchua siri zote za wanadamu sawasawa na matendo yao.
🔹ZABURI 139:7-12.
"7 Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
8 Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko.
9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari;
10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika.
11 Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku;
12 Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa.
✔Mungu hadhihakiwi, ujanja ujanja unaoufanya utaufanya hadi lini? Utaendelea kuigiza hadi lini rafiki? Badilisha muelekeo wako. Acha wokovu wa kuigiza kuna OLE kwa wote wanaofanya UNAFIKI!
kama unakaa kwenye wokovu kaa kwa kumaanisha...
No comments:
Post a Comment