Wednesday, January 17, 2018

UDUNIA

UDUNIA
(1 yohana 2:15-17)
Neno dunia linalotumika hapa halimaanishi sayari ile ambayo wanadamu tunaishi lakini ni zaidi ya maana hiyo, kuna maneno matano ya kiyunani yanayotafsiri dunia/ulimwengu
1/Ge
2/aion
3/aionios
4/oikoumene(hii ndiyo sayari tunayoishi)
5/Kosmos(leo tutaliangalia hili zaidi)
Katika mistari hapo juu katika lugha ya kiyunani unakuta neno Kosmos(yaani msiipende Kosmos wala mambo yaliyo katika Kosmos)
(2Timotheo 4:10) Dema aliniacha akiipenda KOSMOS.
Kuipenda Kosmos ni kuishi maisha ya udunia
(Yohana 14:30) Mkuu wa Kosmos ni shetani mwenyewe (2Wakorintho 4:3-4) m ndogo inamzungumzia shetani, yana anaitwa mungu wa dunia hii.jina lake kiyunani ni KOSMOKRATOR.Nyuma ya udunia(kosmos) kuna huyu kosmokrator.
KOSMOS(dunia) ina maana nyingi ambazo zimefichika
Katika mambo ya udunia yapo ambayo ni dhambi moja kwa moja na mengine yaweza kuwa mazuri lakini yakawa kosmos.
Moja ya mambo ya dunia

1/Mapambo ya Uzuri
Kutokana neno Kosmos tunapata neno la kiingereza "cosmetics" (1 Petro 3:3-6)(Isaya 3:16-24)(kutoka 33:1-6)
Mapambo yoyote kwa mwanamke ambayo yanalenga kuwavuta wanaume kwa uzinzi na uasherati, ili aonekane ni mzuri, anavutia, hivi vyombo vyote vya uzuri nyuma yake yupo kosmokrator, mtu atajichubua ngozi, na kosmokrator anaweza akawatumia wachache kuanzisha mitindo(fashion) na wengine wataiga mfano watu wanavaa milegezo kwa sababu waliwaona watu wanafanya hivyo(Warumi 12:2) "Do not be conformed with fashion of this world. Hatutakiwi kufuatisha namna(mitindo) ya dunia hii mana nyuma yake kuna Kosmokrator(Yakobo 4:4) tukiwa na urafiki na udunia tumekuwa adui wa Mungu(1 yohana 5:4)(1 yohana 2:15-17). Ndani ya dunia kuna kiburi cha uzima, kuna vitu unaweza ukafanya kwa sababu wewe ni mzima, kuna mahari mtu huugua sana hata haoni maana ya vitu hivyo.
Kuipenda dunia kuanaambatana na tamaa
Moja ya sehemu ambayo kuna kosmos ni mitandao(kutumia muda mwingi mitandaoni kuliko maombi au kazi ya Mungu) (Wakolosai 3:1-2)(yohana 17:14-16)
Roho ya kosmokrator ndo ipo nyuma ya michezo yote hii ya dunia, mipira, riadha n.k. watu hushughulishwa na michezo hiyo hata hukosa muda wa kumuhudumia Bwana.
Michezo ya kompyuta(games), karata, draft, bao
(Mathayo 13:22)Biashara, kazi, magari, pikipiki zinazokufanya ushughurishwe hata kukosa ibada kuliko kumpenda Mungu zote hizo ni kosmos(Mwanzo 19:31)(Waefeso 2:2)
(Wafilipi 3:19). Wakati mwingine tumbo nalo linaweza kutufanya tuwaze tu chakula kuliko kumuhudumia Bwana
TUNAUSHINDAJE UDUNIA.
Ni kwa kuwezeshwa na Yesu
Kwanza tunatubu kwa kumaanisha kuacha udunia
Baada ya kuzaliwa mara ya pili tunamwambia Yesu atufanye kuwa kama yeye.ili tuweze kuishinda dunia.

#BishopKakobe

Imeandikwa na Fredie Haule.

No comments:

Post a Comment