Friday, January 19, 2018

KUVAA WIGI NI KUABUDU SANAMU.

ANAE VAA NYWELE BANDIA(WIGI) ANAABUDU MIUNGU BILA KUJUA..

Kama ulikuwa hufahamu ni kwamba mawigi kwa asilimia kubwa yanatokana na nywele za wahindi.

Nywele hizi zinatokana na hekalu moja kubwa sana na maarufu sana India linaloitwa VENKATESWARA TEMPLE, ambapo wanamuabudu mungu(sanamu) wanaemwuita vishnu au lord balaji»» angalia www.tirumala.org«««.

Kinachofanyika sasa ni kwamba wahindi wengi hutoa sadaka nywele zao kwa hio miungu yao kwa  kunyolewa nywele zote na kuwekwa kwenye mapipa maalum, baadae  ndio zinanunuliwa na makampuni wa urembo kisha hutengenezwa wigi. Na wanasema katika mtandao makampuni haya kuwa wanatengeneza haya mawigi, kwa watu wanaojiona  duni vile Mungu amewaumba, ili wafunike nywele zao kwa kuvalia wigi juu yake.

BIBLIA INASEMA NINI JUU YA KUTOA SADAKA KWA MIUNGU

MUNGU anasema watu wanaotoa sadaka kwa miungu wanatoa kwa kwa mashetani na anatuonya vitu vyote vilivotolewa sadaka kwa mashetani tusivishiriki kwa namna yeyote {1WAK 10:14,19-22, KUM 32:17, ZAB 106;37}

Watu zaidi ya million 20 hukatwa nywele zao katika hekalu hilo kila mwaka, sasa emu tujiulize ni wanawake wangapi wanavaa hivo nywele bandia leo? Ni wangapi wanaingia makanisani na nywele zilizotolewa sadaka kwa miungu? Ni Mungu yupi wanaemwabudu, aliewapa nywele wakaona hazifai au wale miungu wanaotolewa sadaka za nywele?

Kwa kuvaa wigi hata kama umeokoka unajiungamanisha moja kwa moja na ibada ya miungu na wengi sana ni vipofu katika hili BWANA ATUSAIDIE KIZAZI HIKI,WENGI WANAPOTEA!!

Mwanamke nywele ni fahari (utukufu)kwako katika uhalisi wake 1WAK 11:15. Unapovaa nywele za mtu mqingine maana yake  unaungamanishwa nae katika ibada yake angalia KUMBUKUMBU 7:26. BWANA AKUPE UFUNUO ILI UTOKE KATIKA KUABUDU MIUNGU, NA UMUABUDU MUNGU ALIEKUUMBA HIVO ULIVO.

             GO NATURAL,AMEN.

Wednesday, January 17, 2018

KWAKO KIJANA-MUHIMU

KWAKO KIJANA;

Hii inakuhusu wewe kijana ulieokoka au ambae hujaokoka.tafadhali soma hadi mwisho kwa kutafakari.

Mtume Paulo katika waraka wake  kwa Timotheo anamwambia hivi, ‘Mtu awaye yote ASIUDHARAU ujana wako, bali uwe KIELELEZO kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.JITUNZE nafsi yako, na mafundisho yako. DUMU katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo UTAJIOKOA NAFSI YAKO NA WALE WAKUSIKIAO PIA’ (1Timotheo 4:12 & 14).
Sentensi hizi zinatuonyesha kwamba kijana yeyote ambaye amefanya uamuzi wa kuokoka, kwa hakika amefanya maamuzi ambayo yanamtaka amaanishe katika kumfuata kwake Yesu au kuuishi wakovu wake. Pamoja na kumpa Yesu maisha yake ni lazima kijana afanye maamuzi ya kuishi maisha ya kudumu kumpendeza Mungu kwa kuzikubali gharama zinazohusiana na wokovu aliouchagua na si kuishi maisha yenye kupelekea jina la BWANA kutukanwa kama ilivyo kwa baadhi ya vijana wengi leo.
Ukisoma mstari huu wa 1Timotheo 4:14.

Jambo muhimu ambalo Mtume Paulo alikuwa akilisisitiza hapa ni hili; jambo muhimu si tu kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wako, bali kila mwamini ana kazi kubwa ya kufanya ili KUULINDA NA KUUTUNZA WOKOVU WAKE.

Moja ya changamoto kubwa sana ambazo zinawakabili vijana wengi waliokoka leo ni kuipenda dunia. Kuipenda dunia kumekuwa tanzi kwa vijana wengi na kwa sababu ya kuipenda dunia; 

(a) Mahusiano ya vijana wengi na Mungu wao yameharibika 
(b) Maisha ya vijana wengi yamekosa uelekeo 
(c) Kutokana na uovu wao jina la Bwana Yesu limekuwa likitukanwa.

Katika kile kitabu cha 1Yohana 2:16 ni dhahiri kwamba dunia imejaaTAMAA YA MWILI, TAMAA YA MACHO NA KISHA KIBURI CHA UZIMA. Tamaa ina nguvu ya kuvuta pamoja na kudanganya, naam inamuingiza mtu kwenye jaribu. Hii ina maana tamaa ni mlango, naam mlango huu unapaswa kufungwa mapema usikupoteze.
(Samweli 11:1-2). Hapa Tunaona anguko la Daudi lilisaabishwa na kumpa Ibilisi nafasi kwa kutokwenda vitani. Mkristo akipoa katika kuvipiga vita vya kiroho inakuwa rahisi kwake kuanguka dhambini (Yakobo 1:14-15), na kumbuka kwamba siku zote tamaa inalenga kumfurahisha mtu binafsi (self-pleasing) bila kujali matokeo yake.

Hivyo katika nyakati tulizonazo sasa suala la kuipenda dunia ni lazima litafutiwe ufumbuzi wa kudumu miongoni mwa vijana wetu. Ujumbe huu mfupi unalenga kueleza kwa namna gani kuipenda dunia kumekuwa tanzi kwa vijana na nini vijana wafanye ili kuikabili na kuishinda changamoto husika.
Pia katika  2Timotheo 2:15 Mtume Paulo anaendelea kumwambia kijana Timotheo ‘Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu,mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli’.

Pengine kila mmoja wetu atafakari maisha yake kwa kuhusianisha na maelekezo ya Paulo kwa Timotheo. Naomba jiulize na kujijibu kwa uaminifu kwamba mosi, je, ujana wako wako unaheshimika au unadharauliwa? Pili, je, kwa waamini wenzako umekuwa kielelezo cha kweli kwa habari ya imani, upendo, usafi, usemi na mwenendo au la?


Naam katika kusoma na kutafakari neno la Mungu nimejifunza kwamba zifuatazo ni njia ambazo zitatusaidia sisi vijana wa leo kuifikia kweli hii ya neno la Mungu.

1. Kijana adumu katika kuomba na kusoma (kutafakari + kulitenda) neno la Mungu.

Katika Zaburi 119:9 & 11 Biblia inasema ‘Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii AKILIFUATA neno lako’. Pia kwenye ule mstari wa 11 inasema ‘moyoni mwangu nimeliweka neno lako, NISIJE NIKAKUTENDA DHAMBI’.
Naam katika Mathayo 26:41 imeandikwa ‘Kesheni, mwombe, MSIJEmkaingia majaribuni; roho I radhi, lakini mwili ni dhaifu’. Yohana 17:17 inasema ‘uwatakase kwa ile kweli ;neno lako ndiyo kweli. Mambo haya mawili yanapaswa kwenda kwa pamoja nakijana akidumu katika kuomba na kusoma neno la Mungu ushindi ni lazima.

2. Kijana asimpe Ibilisi nafasi.

Kijana anapaswa kujiuepusha na mazingira yenye kumfanya aiepende na kuifuatisha namna ya dunia hii.
Katika kitabu cha 1Wakorinto 6:12 imeandikwa ‘Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote VIFAAVYO; vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya UWEZO wa kitu chochote’.  Ni vizuri ukahakikisha kwamba ufahamu wako hautawaliwi na mambo yasiyo ya msingi– Je ufahamu wako umetawaliwa ni nini??
Hii ndiyo sababu iliyomfanya Paulo awaambie Waefeso ‘Wala msimpe Ibilisi nafasi’ (Waefeso 4:27) na pia awaambie Warumi “Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili hata kuwasha tamaa zake’ (Warumi 13:14).
➡ Je hivi leo ni kwa namna gani vijana wanaungalia mwili na kumpa Ibilisi nafasi? – Mitandao ya kijamii, kuangalia na kusoma vitu vichafu, hasira, mawazo, mazingira.

Mfano wa Vijana
3. Kijana azikimbie tamaa za ujanani.

Katika 2Timotheo 2:22 imeandikwa ‘LAKINI ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi’. Kijana anawezaje kuzikimbia tama za ujanani?angalia mfano wa Yusufu. Ushindi wa Yusufu dhidi ya mke wa potifa (Mwanzo 39:2-9). 

Hii ni habari ya kijana Yusufu ambaye alikuwa msimamizi mkuu wa mali za Potifa.
Pamoja na ushawishi aliokutana nao Yusufu alijibu kwamba ‘Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?’ Mwanzo 39:12 inasema ‘huyo mwanamke akamshika nguo zake, akisema, Lala nami. Yusufu akaiacha nguo yake mkononi mwake akakimbia akatoka nje. Ili kuzikimbia tamaa za ujanani kijana anapswa,

(a) ajiepushe na mazingira/marafiki wabaya (Mithali 1:10 & 1Wakorinto 15:33).

(b) Ajitenge na uovu (Mithali 16:17, Zaburi 1:1).

Ni muhimu ukakumbuka kwamba hukupewa mwili kwa ajili ya zinaa maana miili yenu ni ni viungo vya Kristo na tena hekalu la Roho Mtakatifu (1 Wakorinto 6:15 & 19), tena yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye (1 Wakorinto 6:17) maana tena imeandikwa ‘Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili’ (1Wakorinto 6:13b). Tena imeandikwa ‘Lakini uasherati USITAJWE kwenu kamwe, wala uchafu wowote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu’   (Waefeso 5:3)
Rafiki, mkimbilie Yesu leo akuwezeshe kuishi maisha yanayompendeza maana unazo nguvu za kumshinda ibilisi.

  BWANA AWABARIKI SANA.

Na Isaiah membe, mtumwa wa Kristo.

KUWAOMBEA WATU KWA FEDHA

WANAPOTEA KWA KUWA HAWAYAJUI MAANDIKO-KUWAOMBEA WATU KWA FEDHA.
Yesu alisema nyakati za mwisho kutakuwako mitume na manabii wa Uongo MAT 24:24 ambao watapoteza wengi hata waliowateule. Lakini pia alisema watu watakuwa wenye kupenda fedha kuliko kumpenda Mungu, 2TIMOTHEO 3:1-2.

Lakini katika UFUNUO 2:2 anasema tuwajaribu hao wajiitao mitume ili tujue kuwa ni waongo au namna gani, Mungu pia anasema tuzijaribu hizo roho tuone kama zinatokana na Mungu au La! tunawapima kwa NENO LA MUNGU.

Kuna wimbi kubwa la watu ambao wanatajwa ni watumishi wa Mungu, wanafanya maonbezi kwa watu kwa kuwatoza fedha. utaskia Mambo kama haya;
*kumuona mchungaji sh.10000.
*kuombewa ugonjwa fulani Sh.100,000 na mengi yanayofanana na hayo!

Maombezi yote ya uponyaji wa kibiblia kamwe hayafanyiki kwa fedha {MATHAYO 10:7-8.}

Karama zote tunazozipokea kutoka kwa Mungu, Mungu anatupa bure kabisa hakuna anaemlipa Mungu ili apate karama yeyote ile.

Neno KARAMA kama linavotajwa katika 1wakorintho sura ya 12 katika lugha ya asili linamaanisha ZAWADI (gift of the holy spirit).
Zawadi mara zote inatolewa bure bila kuilipia chochote.

Wokovu pia ni karama ambao tunaupokea bure Inayotupa uzima wa milele. Ukisoma andiko hili la WARUMI 6:23 kwa kiingereza utaona neno, THE GIFT OF ETERNAL LIFE.
Tunahesabiwa haki bure katika kristo Yesu pekee, WARUMI 3:23-24.

Sasa mtu anaombea watu kwa fedha, inabidi na mtu akitaka kuokoka basi amtoze afanye hivohivo amtoze pesa pia. Kama haiwezekani na hawafanyi hivo wanapowataka watu waokoke, basi na uponyaji ni vilevile, inawapasa kuwaombea watu bure bila fedha yeyote {ZABURI 103:3}

Yeyote anaeombea watu kwa fedha sio mtumishi wa Mungu alie hai hata kama ni mtu HUYO anajiita nabii,mtume,askofu na jina lolote lingine.

Uponyaji wote Yesu kaulipia na kuugharamia kwa kazi alioifanya msalabani aliposema yote yamekwisha( IT IS PAID IN FULL).Uponyaji wa magonjwa yote umeshalipiwa ,huna haja ya kutoa fedha kwanza ndio uombewe. Kufanya hivo ni kutokuifahamu Kweli ya NENO.

Watumishi wa Mungu wa nyakati za biblia walikuwa hawaombei watu kwa fedha mfano:

NABII ELISHA ,2WAFALME 5:13-18,20-27.

MTUME PETRO, MATENDO8:9-24.

Na mitume wote na nyakati za kanisa la kwanza.

Acha kudanganywa na mitume na manabii Hawa feki ambao ni maajenti wa ibilisi, hawana tofauti na GEHAZI mtumishi wa elisha, wamejaa uongo mwingi sana, utaskia wanasema "Bwana amesema na mimi, unipe gari lako" "Bwana amesema nami unipe nyumba yako" na mengi tu mengine yanayofanana na hayo.

Maandiko yanasema hizi ni nyakati za hatari,wengi watajitenga na imani wakiskiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani 1TIMOTHEO 4:1, 2TIMOTHEO 3:1.

Itafute KWELI ya NENO la MUNGU, IKUWEKE HURU ili  usije ukachukuliwa na roho hizi za nyakati za mwisho.

Bwana akubariki sana.

Isaiah Membe,Mtumwa wa Kristo.

KIPIMO SIO KWENDA KANISANI.

KIPIMO SIO KWENDA KANISANI

Watu wengine siku za ibada kama Jumapili au jumatano, wanakuwa katika mambo yao wenyewe, wengine watakuwa bar, wengine shambani, wengine kwenye biashara zao nakadhalika. 

Kutokana na hili sasa wengi watawachukulia wale wanaokwenda kanisani kuwa ndio watu wa Mungu Na wale wasioenda ni watu wa shetani.

Lakini jambo hapa la kufahamu ni kuwa hata  katika kundi hilo la watu waendao kanisani kuna wengi pia ambao wako mbali sana na Mungu.
Wengine wanaenda kanisani kupotezeza Muda tu, wengine kutafuta wachumba, wengine kutafuta uponyaji, wengine kutafuta baraka tu nakadhalika.

Bwana Mungu anasema watu hawa wanaenda ibadani na hukaa kama watu wa Mungu lakini sio watu wanaompenda Mungu. EZEKIEL 33:30-33. MARCO 7:6.

Sikiliza kipimo si kwenda kanisani, kipimo sio kuhubiri wala kufundisha, Kipimo sio kujionyesha kwa watu kwa unafiki tu LAKINI  Kipimo ni kuishi MAISHA YAKO sawasawa na NENO la MUNGU.(ZABURI 119:6,9).

Wengi wa hao waendao makanisani hawalifurahii NENO la MUNGU, kwa sababu silo walilolifata hapo, hawataki kukemewa Maovu yao wala hawataki kuonywa KINYUME chake wanapenda MANENO LAINI YADANGANYAYO, ISAYA 30:9-11.

Wako wengi wanaenda kanisani lakini hawataki maisha yao ya dhambi yaguswe Kabisa katika mahubiri kwa sababu Ndani yao hamna kitu, wako kanisani kwa Lengo lingine kabisa!
Kuwa watu wa Mungu ni vile tunavolitii na kulifurahia  neno la Mungu (ZABURI 119,9,103), Vile tunavyokuwa Tayari kukemewa na kuonywa kwa Neno la MUNGU (ZABURI 119:105), Kuwa mtu wa Mungu ni jinsi gani tunavyonyenyekea na kuwa tayari kuongozwa na NENO la Mungu.

Ukisema unampenda Mungu wakati neno lake hulipendi  ambalo Ndilo hasa linalotusafisha na kututakasa (YOHANA 17:17), NENO ndilo linagusa maisha yako ya dhambi na kuweka wazi uchafu wote wa uovu na kutufanya Kutubu, KAMA HULIFURAHII NENO rafiki, HAPO hakuna kumpenda Mungu, 

kumpenda Mungu ni kuzishika amri zake YOHANA 14:21,23-24. wakati unakuja ambapo Magugu na ngano vitatengwa.Maana Yesu alisema yaacheni magugu na ngano vikae pamoja ila wakati unakuja atakapoyatenganisha magugu na ngano na hapo ndipo itakuwa wazi nani alikuwa MBUZI na nani alikuwa KONDOO, 

USIKUBALI KUWA katika kundi la Mbuzi au Magug,  Kama unaamua Amua kuwa mtu wa Mungu kweli kwa Kumaanisha kulishika Neno lake lote bila kuchaguachagua ya kushika na yanayokugharimu unayaacha.ZABURI 119:6,9,11,98-100.

Ubarikiwe sana.

Isaiah Membe,Mtumwa wa Kristo.

NINI MAANA HALISI YA KUFUNGA.

NINI MAANA HALISI YA KUFUNGA.

wako baadhi ya watu Katika  kipindi cha KWARESMA kwa mujibu wa imani yao huwa wanakuwa wanafunga kwa namna fulani fulani, lakini yako mambo ya kujifunza hapa⤵⤵

Neno “KUFUNGA“ linatokana na neno la Kiyunani “NESTEVO“, ambalo nalo linatokana na maneno mawili ya Kiyunani “NE“ na “ESTHIO“.  Neno “NE“ maana yake “BILA“ au “HAPANA“, Kiingereza “NO“ au “WITHOUT“.  Neno “ESTHIO“ maana yake “KULA CHAKULA AU KINYWAJI“, Kiingereza “TO EAT SOLID OR LIQUID FOOD“. 

Neno “NESTEVO” sasa linaunga maneno hayo mawili ya Kiyunani ”NE” na “ESTHIO”, na lina maana “BILA KULA CHAKULA AU KINYWAJI CHOCHOTE”.

➡  Hivyo maana ya kufunga, ni “BILA KULA CHAKULA AU KINYWAJI CHOCHOTE”.

Kufunga siyo kuacha kusoma gazeti ulilozoea, kuacha kuchana nywele n.k., ni kuacha kabisa kula au kunywa kinywaji chochote.  Maana hii ya kufunga, inathibitishwa na maandiko yafuatayo:- EZRA 10:6; YONA 3:7; 2 SAMWELI 3:35; ESTA 4:16; KUMBUKUMBU LA TORATI 9:9; MATENDO 9:9.

Kufunga siyo kuacha kula vyakula kama ugali au wali halafu ukawa unakunywa soda, maziwa, uji au kula matunda n.k. Ni kuacha kula chochote wala kunywa chochote kile.  Andiko linalotumika kuhalalisha kula vitu vidogo vidogo ni DANIELI 10:2-3.  Katika andiko hili “SIKULA CHAKULA KITAMU”, chakula kitamu ni “DESSERTS” kwa Kiingereza au “PUDDING” – ndizi, nanasi, papai, machungwa n.k.
✔  Katika mistari hiyo Danieli anasema hakula lolote kabisa.

Kwa hio kama tunafunga lazima kuacha kula kwa muda fulani kulingana na ratiba yako kuwa unafunga kwa muda gani, masaa 12, 24 n.k.

™Neno from Bishop Zachary kakobe.

AMKENI USINGIZINI.



(Chungu lakini inaponya!!).

Ujumbe  unatoka:  ISAYA 56:10-11,

"Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana MAARIFA; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala usingizi. Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na ni WACHUNGAJI wasioweza kufahamu NENO; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote".


Giza nene la Kiroho linazidi kuisonga dunia yetu kwa sababu ya viongozi wa dini, na watu wengi sana wataangamia siku ya mwisho kwa sababu ya kupotoshwa na viongozi. Neno linasema HOSEA 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani wangu mimi; kwa kuwa umeisahau Sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahu watoto wako”

Kizazi chetu kiko kwenye hatari kubwa, kwani Shetani ametunga falsafa nyingi za uongo, juu ya kweli ya NENO la MUNGU.

Wapendwa! Amkeni pambazuko liko karibu, mnapoona Dini na Madhehebu mengi yakianzishwa huku kila mmoja akiwa na mafundisho tofauti na mengine yaliyo kinyume neno la Mungu, jueni unabii unatimia, ukibahatika kuufahamu ukweli, CHANGAMKA! amua kuufuata ukweli. 

Mungu anasema ISAYA 9:16“Kwa maana wawaongozao watu hawa ndio wawakoseshao, na hao walioongozwa na watu hao wameangamia” .

Hapa hakuna usalama, Wachungaji wasiojua kweli ya Mungu na Waumini wao wanaokubali chochote bila kuchunguza ukweli, wote wataangamia.


Ujumbe huu ni sauti ya Matengenezo kwa kila anayejiita Mtumishi, bila kujali cheo chake Wala wadhifa wake. 

Neno linasema; wachungaji wamekuwa ni sawa na Mbwa Bubu asiyebweka adui anapovamia zizi la kondoo, hebu jiulize – Inakuwaje Uovu unadumu kati ya waumini? Kama Mtumishi anazini na waumini, au ni mlevi, muuza madawa ya kulevya n.k. waumini watakuwaje?Tunaona, Kwa sababu ya Maslahi! wenye pesa makanisani na miskitini hawakemewi hata kama wanafanya Dhambi za wazi, Viongozi wamepofushwa macho kwa sababu ya Maslahi.

Oooh! Wapendwa; wakemeaji wa dhambi siku hizi wako wapi?? Manabii na waonyaji, kama akina Isaya, yeremia, Hosea, Ezekiel n.k. wako wapi siku hizi? Mbona wote wamegeukia Injili ya UTAJIRI na Kujikusanyia watu wenye Pesa kwa ajili ya maslahi yao binafsi?


Wakati wote wanafundisha Ujumbe laini, mafundisho yadanganyayo, wanikazia - uponyaji, utajiri, Baraka, Kupanda mbegu, Zaka na sadaka, amani n.k. huku waumini wakidumu kwenye Dhambi na hatimaye kuingia kwenye maisha magumu zaidi ya walivyokuwa mwanzo. 

aKatika historia ya Biblia hakuna Nabii wala Mtume aliyekuwa na Injili ya akijilimbikizia Mali za Dunia hii kwa mgongo wa injili na sadaka za waumini, mbali na Kuonya na Kukemea dhambi.

Hebu jiulize Wewe mchungaji: Je Ni kweli wewe umetumwa na unaongozwa na Mungu KWELI?

Huo ulevi, Hiyo tamaa ya Ngono, huko kupenda Fedha na utajiri, Hiyo mipango unayoungana na Dini ya mashetani kupinga kweli ya Mungu, huo upendeleo kwa wenye Pesa na kudharau maskini, na hiyo nyumba ndogo ULIONAYO, na huyo bwana asiye mume wako, na hayo madawa ya kulevya na biashara haramu.

huo utapeli na udanganyifu, na huko kugombania madaraka na kufanya kampeni kama vyama vya siasa, hiyo michezo michafu ya kuchezea mabinti za watu,na hizo hirizi unazotumia kuvuta watu na kutenda miujiza ukihadaa roho za watu kwa jina la Upako, hizo hasira,chuki, visasi na Mambo yanayofanana na hayo; Unaamini yanatokana na Roho Mtakatifu??.

MSIDANGANYIKE; Mungu anasema “Tokeni kwake (Shetani na Mpinga Kristo), enyi watu wangu, msishiriki Dhambi zake, wala msipokee mapigo yake” Ufunuo 18:4. TOKENI HARAKA YESU ANARUDI, KWA WATEULE!!!!

Mbwa mwitu wamevamia kundi, nani wa kusimama kupiga kelele, wakati utitili wa mafundisho potofu yaliyo kinyume na ukweli wa neno la Mungu yanaiingia kanisani!  nani wa kutoa maonyo na kutengeneza? Neno linasema 2TIMOTHEO 4:2-4 “Lihubiri NENO, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, KARIPIA, KEMEA, na KUONYA kwa uvumilivu wote na mafundisho. Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundsho yenye uzima … na kuzigeukia hadithi za Uongo” 

 "Neema imefunuliwa ili kutuweka HURU mbali na Dhambi", sio kuhalalisha dhambi, kama wengi wanavyodai, huku wakizidi kuzama katika matope ya Dhambi. Washirika kueni makini mnaweza kujikuta mnatumbukizwa shimoni na kupotea milele katika jehanam ya moto na kisha ziwa la Moto kwa kuzifanya shingo zenu kuwa Ngumu. AMKENI ITAFUTENI KWELI YOTE, NYAKATI HIZI NI ZA HATARI SANA,kilaa mmoja ajiangalie mwenyewe na kuutimiza wokovu wake kwa kuogopa na kutetemeka.WAFILIPI 2:12.


GOATU

JE, UNAJUA G.O.A.T.U. NI NINI?

✔Wanachama wa Kikundi cha siri cha freemason wanamwabudu mungu
anayeitwa GAOTU – Great Architect Of The Universe – yaani ‘Mbunifu mkuu wa
ulimwengu.’ Freemason hawamwabudu Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
Sala zao zote huelekezwa kwa GAOTU.

✔Architect ni mtu anayebuni ramani za majengo,
majengo unayoyaona katika nchi mbalimbali yakiwemo yale yaliyomo ndani ya miji ya
nchi yetu, yanatokana na ubunifu wa watu wanaoitwa Architects. Ni watu wenye elimu
kubwa sana kuhusu mambo ya ubunifu na ujenzi wa majengo.

✔Freemason nao ni
wajenzi wa maadili wanayoyataka wao na pia wanaye Architect (mbunifu) wao mkuu
ambaye ndiye wanayemwabudu, jina la Architect wao ni GAOTU. Huyo ndiye mbunifu
mkuu wa shughuli za Freemason katika ujenzi wa ulimwengu, wengine ni
watekelezaji tu.

✔Wapo watu pia wanaoelekeza sala zao kwa viumbe badala ya kuelekeza kwa Muumbaji. Wao pia hawatofautiani na Freemason maana wote
wanakwenda kinyume na Mungu, na ukweli ni kwamba wanafanya hivyo kutokana na ubunifu wa GAOTU
maana kazi yake ni kubuni mbinu mbalimbali za kuwafanya watu wawe mbali na Mungu.

✔ Yesu anasema kwamba tunapotaka kusali tusali hivi, “Baba yetu uliye
mbinguni……” Mathayo 6:9-13, ikimaanisha kwamba sala zetu zote tuzielekeze kwa
Mungu aliye mbinguni tena kwa Jina la Yesu.
➡ GAOTU anajua kwamba Mungu alisema,
“mtu akijikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote” Yakobo 2:10, ndio maana
anajitahidi kuwafanya watu wamkosee Mungu hata katika kitu kidogo, na watakuwa wamemkosea juu ya yote. Hivyo unaweza ukawa mlokole, msabato, mkatoliki,
muislamu, mbudha, myahudi nk. lakini ukimkosea Mungu katika jambo moja tu
umemkosea juu ya yote.

✔Ndio maana leo hii katika dunia nzima kuna utitiri wa
madhehebu na dini za kila aina. Wataalamu wanasema kuna dini zaidi ya elfu tatu! Je,
wote watakwenda Paradiso? Biblia inasema, “Je! Hamjui ya kuwa wale washindanao
kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja?” 1 Wakorintho
9:24. Hivyo pamoja na kuwa na dini nyingi kiasi hicho na dini zote zikiwa zinadai
kupiga mbio ili kupata tuzo ya uzima wa milele, ni wale tu wanaotii kila moja ya amri za Mungu ndio wanaopiga mbio vizuri na ndio watakaopata tuzo, nao watatoka katika dhehebu moja tu.

✔Kwa nini watu huingia Freemason? Ni kwa sababu ya kutaka utajiri wa dunia hii.
➡Wakati shetani anamjaribu Yesu, alimwonyesha utajiri, “Kisha ibilisi akamchukua
mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.” MATHAYO 4:8, 9.
✔Baada ya ibilisi kushindwa kumnasa Yesu, sasa aliendelea kutumia njia hiyo hiyo kwa kumtumia mnyama ili awape watu utajiri kupitia Freemason, ➡tunasoma kwamba, “Lakini katika
mahali pake atamheshimu mungu wa ngome; na mungu ambaye baba zake hawakumjua
atamheshimu, kwa dhahabu na fedha, na vito vya thamani na vitu vipendezavyo…..na
yeye atakayemkubali atamwongeza kwa utukufu; naye atawapa kumiliki wengi; naye ataigawa nchi kwa rushwa.” Danieli 11:38,39. Ndio maana watu wengi wanaingia kwenye vyama vya siri kama Freemason na kila anayeingia humo hufanywa apate Kumiliki vitu vingi na kuwa tajiri mkubwa.
➡➡Ni sehemu ndogo ya neno la uzima kutoka kwa mtumishi wa MUNGU, ASKOFU ZACHARY KAKOBE. Ukitaka kulisoma somo hili kwa mapana na marefu na kufahamu siri nzito kuhusu FREEMASONS NA ILLUMINATI ingia kupitia link hii⤵⤵
➡www.davidcarol719.wordpress.com/freemasons-na-illuminanti/
UBARIKIWE NA BWANA.